Waziri wa fedha aigomea polisi nchini Afrika Kusini

Share it:

Waziri wa fedha wa Afrika Kusini, Pravin Gordhan, amegomea mwito wa polisi nchini humo waliomtaka kuripoti kituo cha polisi, na kusema kwamba tuhuma dhidi yake hazina msingi.
Bwana Gordhan ameeleza kuwa timu yake ya kisheria ilimshauri kutoitikia mwito huo na kwamba yeye alikuwa akitimiza wajibu wake kama kawaida.
Vyombo vya habari nchini Afrika Kusini zinaeleza kuwa sababu ya mwito huo zinatokana na uchunguzi uliofanywa dhidi ya kitengo alichowahi kukisimamaia cha masuala ya kodi ambacho kinashutumiwa kwa kuwachunguza wanasiasa nchini humo.
Upande wa upinzani unahisi kuwa waziri huyo ni mwathirika wa jaribio la kumdhoofisha linalofanywa na wafuasi wa Rais Jacob Zuma.

Share it:

Unknown

Breaking news

Post A Comment:

0 comments:

Also Read

Lil Wayne Sparks Music Deal with Pot Biz ... 'Cause It's 4/20 and Stuff

Lil Wayne may be the one stoner today who is actually productive -- he just dropped a new music vid on the holy day of p

Unknown