Jinsi polisi wanne walivyouawa Dar

Share it:

ASKARI wanne wa Jeshi la Polisi wameuawa kwa kupigwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi baada ya kuwavamia wakati wakitekeleza majukumu yao.

Katika tukio hilo lililotokea Benki ya CRDB iliyopo Mbande, Mtaa wa Magengeni, Kata ya Chamazi wilayani Temeke, Dar es Salaam juzi, pia raia wawili wamejeruhiwa.

Kwa mujibu wa mashuhuda, majambazi hayo yalianza kuwashambulia kwa risasi askari walipokuwa wakikabidhiana lindo majira ya saa 1 usiku.

ASKARI WALIVYOVAMIWA

Akizungumza na MTANZANIA katika eneo la tukio jana, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Magengeni, Sadick Makanwa, alisema hakuna mtu aliyewatambua majambazi hao wakati wanafika eneo hilo kwani walikuwa wamevalia mavazi ya kawaida.

Alisema kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, askari walifika wakiwa na gari lao aina ya Noah lenye namba PT 3889 na kuliegesha mbele ya jengo la Benki ya CRDB.

“Ilikuwa majira ya saa 1:15 hivi, askari walikuja na gari yao na kuigesha mbele ya benki. Kama ilivyo kawaida yao huwa wanabadilishana lindo inapofika jioni.

“Askari mmoja alifungua mlango na aliposhuka toka kwenye gari, ghafla wakaanza kushambuliwa kwa risasi ambazo hakuna aliyejua zinatokea upande gani.

“Yule askari alianguka na dereva naye alishambuliwa akiwa ndani ya gari na kupoteza uhai palepale,” alisema Makanwa na kuongeza:

“Wakati huo kulikuwa na askari mwingine alikuwa anatoka ndani ya benki kwenda kuwapokea wenzake, alipoona mwenzake ameanguka, alianza kukimbia. Lakini ghafla naye alipigwa risasi ya kichwani akaanguka.”

Alisema askari mwingine aliyekuwa ndani ya benki alitoka na alipoona wenzake wapo chini, aliamua kukimbia na kutumia upenyo uliokuwa baina ya kibanda cha walinzi na ukuta wa jengo la benki, na kwenda kujificha kwenye nyumba ya udongo iliyokuwa mbali na eneo la tukio.

Makanwa alisema watu hao walikimbia kuelekea upande wa kulia karibu na kituo Kidogo cha Polisi ambapo walikuwa wameegesha pikipiki zao.

WALIVYOTUMIA PIKIPIKI

Alisema kwa mujibu wa mashuhuda, pikipiki hizo zilikuwa tatu na hazikuwa na namba za usajili.

“Walipakizana watatu watatu kwenye pikipiki mbili na wawili wakapanda kwenye pikipiki moja.

“Waliweka silaha zao kwenye kiroba na kuelekea upande wa kulia wa benki hadi karibu na kituo kidogo cha polisi ambako walikuwa wameegesha pikipiki zao,” alisema.

Alisema walitumia mbinu ya kujifanya wao ni raia wa kawaida wakisikika wakisema ‘wamekimbilia huku’, ili wasitambulike kama ndio waliofanya unyama wa kuua askari.

“Baada ya kupanda pikipiki, majambazi wawili waliokuwa na bastola walikaa nyuma ya pikipiki na walikimbia kuelekea Barabara ya Serengeti,” alisema Makanwa na kuongeza kuwa tukio hilo lilidumu kwa dakika saba hadi 10.

Makanwa alisema baada ya kufanya unyama huo, majambazi hao waliiba silaha na hawakuingia ndani ya benki kuchukua fedha.

“Hili tukio kwa namna lilivyotokea, inaonekana hawa watu walikuja muda mrefu na kujificha wakisubiri askari wafike ndipo wawavamie na kuwapora silaha, hawakuwa na nia ya kuiba fedha” alisema.

Shuhuda mwingine aliyejitambulisha kwa jina moja la Abdallah, alisema wakati tukio hilo linatokea, alikuwa ndani ya mgahawa wake uliopo jirani na benki hiyo.

“Nilisikia mlio wa risasi, sikushtuka, nilifikiri ni askari ‘wameshtua’ kwa sababu huwa siku moja moja wanafyatua risasi. Lakini ghafla nilisikia kishindo ukutani karibu na dirisha, nikagundua ni risasi.

“Nililala chini, risasi ziliendelea kufyatuliwa kwa dakika kama tano kisha zikatulia. Nilianza kutambaa kuelekea chumbani, mara zilianza tena kufyatuliwa kwa dakika nyingine kama tano,” alisema Abdallah.

Shuhuda mwingine ambaye ni mmoja wa majeruhi, Aziz Yahaya, alieleza kuwa tukio hilo lilitokea akiwa kazini kwake, mita chache kutoka ilipo benki hiyo.

“Nilikuwa katika shughuli zangu za kila siku za kuuza mgahawa. Walikuja wateja wawili mtu na mke wake wakiwa na mtoto, wakaagiza chipsi mayai. Baada ya muda kidogo nikiwa nawandalia, nikasikia mlio wa risasi.

“Sikutilia maanani kwa sababu nilifikiri ni polis

Share it:

Breaking news

Post A Comment:

0 comments: